SAMSONI

Language: Swahili
Nyimbo Za Umoja

SAMSONI

[1]
Samsoni mwenye nguvu nyingi alimpenda yule Delila,
Siku moja alilazimika,
Kuitoa siri ya Mungu.

Samsoni akasema, kwa Delila, akasema,
Sijanyoa nywele zangu, tangu utoto wangu
Nikinyoa nywele zangu nguvu zitakwisha,
Pia mimi Mnadhiri wa Mungu toka tumboni,
Wembe bado kunipita kichwani Delila.

[2]
Na Delila aliona kwamba, amepewa siri kabisa,
Akamwita mtu mmoja aje,
Amnyoe nywele Samsoni.

[3]
Pia sisi wanadamu wote, tusitoe siri ya Mungu,
Na Shetani atatubembeleza,
Mwisho atushinde kabisa.