Cha Kutumaini Sina

Song Lyrics

Cha Kutumaini Sina

Nyimbo Za Umoja · Swahili
Present

Lyrics

Font size:
[1]
Cha kutumaini sina,
Ila damu yake Bwana,
Sina wema wa kutosha,
Dhambi zangu kuziosha.

[chorus]
Kwake Yesu nasimama (Haleluya)
Ndiye mwamba ni salama (Haleluya)
Ndiye mwamba ni salama.

[2]
Njia yangu iwe ndefu,
Yeye hunipa wokovu
Mawimbi yakinipiga,
Nguvu zake ndiye nanga

[chorus]
Kwake Yesu nasimama (Haleluya)
Ndiye mwamba ni salama (Haleluya)
Ndiye mwamba ni salama.

[3]
Damu yake na sadaka,
Nategemea daima,
Yote chini yakiisha,
Mwokozi atanitosha.

[chorus]
Kwake Yesu nasimama (Haleluya)
Ndiye mwamba ni salama (Haleluya)
Ndiye mwamba ni salama.

[4]
Nikiitwa hukumuni,
Rohoni nina amani,
Nikivikwa taji yake,
Sina hofu mbele zake.

[chorus]
Kwake Yesu nasimama (Haleluya)
Ndiye mwamba ni salama (Haleluya)
Ndiye mwamba ni salama.

Support My Songbooks

Help us expand our library and keep the music alive for everyone. Even a small donation goes a long way.

Buy me a coffeeBuy us a coffee