Liko Lango Moja Wazi

[1]
Liko lango moja wazi ,
Ni lango la Mbinguni,
Na wote waingiao
watapata nafasi.

[chorus]
Lango ndiye Yesu Bwana
Wote waingie kwake ,(lango)
Lango,Lango, lango, lango
La Mbinguni ni wazi

[2]
Yesu ndiye lango hili,
Hata sasa niwazi,
kwa wakubwa na wadogo,
Tajiri na maskini.

[chorus]
Lango ndiye Yesu Bwana
Wote waingie kwake ,(lango)
Lango,Lango, lango, lango
La Mbinguni ni wazi

[3]
Hili ni lango la raha,
Ni lango la rehema,
Kila mtu apitaye
hana machozi tena.

[chorus]
Lango ndiye Yesu Bwana
Wote waingie kwake ,(lango)
Lango,Lango, lango, lango
La Mbinguni ni wazi

[4]
Tukipita lango hili
Tutatua mizigo,
Tuliochukua kwanza,
Tutavikwa uzima.

[chorus]
Lango ndiye Yesu Bwana
Wote waingie kwake ,(lango)
Lango,Lango, lango, lango
La Mbinguni ni wazi

[5]
Hima ndugu tuingie
Lango halijafungwa,
Likifungwa mara moja
Halitafunguliwa.

[chorus]
Lango ndiye Yesu Bwana
Wote waingie kwake ,(lango)
Lango,Lango, lango, lango
La Mbinguni ni wazi