Kazi Yangu Ikiisha

[1]
Kazi yangu ikiisha, nami nikiondoka,
Na kuvaa kutokuharibika,
Nitamjua Mwokozi nifikapo ng'amboni,
Atakuwa wa kwanza kunilaki.

[chorus]
nitamjua , nitamjua nikimwona uso kwa uso,
Nitamjua,nitamjua kwa alama za misumari

[2]
Furaha nitapata nikiona makao
Bwana aliotuandalia
Nitamsifu Mwokozi kwa rehema na pendo
Vilivyonipa pahali Mbinguni

[3]
Naowaliokufa katika Bwana Yesu
nitawaona tena huko juu
Lakini nifikapo kwake huko Mbinguni
Nataka kumwona Mwokozi kwanza.

[4]
Milangoni mwa mji Bwana atanipisha
Pasipo machozi wala huzuni
Nitaimba wimbo wa milele; lakini
Nataka kumwona Mwokozi kwanza