Ni Salama Rohoni Mwangu

[1]
Nionapo amani kama shwari
Au nionapo shida;
Kwa hali zote umenijulisha
Ni salama rohoni mwangu

[chorus]
(Salama) salama rohoni,
ni salama rohoni mwangu X2

[2]
Ingawa shetani atanitesa
Nitajipa moyo kwani
Kristo ameona unyonge wangu
Amekufa kwa roho yangu

[chorus]
(Salama) salama rohoni,
ni salama rohoni mwangu X2

[3]
Dhambi zangu zote, wala si nusu
Zimewekwa Msalabani
Wala sichukui laana yake
Ni salama rohoni mwangu

[chorus]
(Salama) salama rohoni,
ni salama rohoni mwangu X2

[4]
Ee Bwana himiza siku ya kuja
Panda itakapolia;
Utakaposhuka sitaogopa
Nisalama rohoni mwangu

[chorus]
(Salama) salama rohoni,
ni salama rohoni mwangu X2