Baragumu Yake Bwana

[1]
Baragumu yake Bwana wakati ikipigwa
Na siku ya milele ikifika;
Hapo waliokombolewa watakusanyika
Nitakuwapo, jina kuitika

[chorus]
Na majina yaitwapo X3
Kuitika jina, nitakuwapo

[2]
Wafu wa Kristo wafufukapo kwa siku ile,
Tutashiriki na fahari yake;
Waliochaguliwa watakaribishwa kwake
Nitakuwako jina kuitika

[chorus]
Na majina yaitwapo X3
Kuitika jina, nitakuwapo

[3]
Saa zote na tumfanyie Bwana kazi yake
Tangu asubuhi hata jioni
Maisha yetu ikomapo humu duniani
Nitakuwako jina kuitika

[chorus]
Na majina yaitwapo X3
Kuitika jina, nitakuwapo