Bwana Mungu, Nashangaa

[1]
Bwana Mungu, nashangaa kabisa
Nikitazama kama vilivyo
Nyota ngurumo vitu vingi vyote
Viumbavyo kwa uwezo wako

[chorus]
Roho yangu na ikuimbie
Jinsi wewe ulivyo mkuu
Roho yangu na ikuimbie
Jinsi wewe ulivyo mkuu

[2]
Nikitembea pote duniani
Ndege huimba nawasikia
Milima hupendeza macho sana
Upepo nao nafurahia

[chorus]
Roho yangu na ikuimbie
Jinsi wewe ulivyo mkuu
Roho yangu na ikuimbie
Jinsi wewe ulivyo mkuu

[3]
Nikikumbuka kama wewe Mungu
Ulivyompeleka mwanao
Afe azichukue dhambi zetu
Kuyatambua ni vigumu mno

[chorus]
Roho yangu na ikuimbie
Jinsi wewe ulivyo mkuu
Roho yangu na ikuimbie
Jinsi wewe ulivyo mkuu

[4]
Yesu mwokozi utakaporudi
Kunichukua kwenda mbinguni
Nitashukuru na kwimba milele
Wote wajue jinsi ulivyo

[chorus]
Roho yangu na ikuimbie
Jinsi wewe ulivyo mkuu
Roho yangu na ikuimbie
Jinsi wewe ulivyo mkuu