Wamwendea Yesu Kwa Kusafiwa

[1]
Wamwendea Yesu kwa kusafiwa,
Na kuoshwa kwa damu ya kondoo?
Je, neema yake umemwagiwa?
Umeoshwa kwa damu ya kondoo?

[chorus]
Kuoshwa, kwa damu
Itutakasayo ya kondoo;
Ziwe safi nguo nyeupe mno;
Umeoshwa kwa damu ya kondoo?

[2]
Wamwandama daima Mkombozi
Na kuoshwa kwa damu ya kondoo?
Yako kwa Msulubiwa makazi,
Umeoshwa kwa damu ya kondoo?

[chorus]
Kuoshwa, kwa damu
Itutakasayo ya kondoo;
Ziwe safi nguo nyeupe mno;
Umeoshwa kwa damu ya kondoo?

[3]
Atakaporudi Bwana arusi
Uwe safi kwa damu ya kondoo!
Yafae kwenda Mbinguni mavazi
Yafuliwe kwa damu ya kondoo?

[chorus]
Kuoshwa, kwa damu
Itutakasayo ya kondoo;
Ziwe safi nguo nyeupe mno;
Umeoshwa kwa damu ya kondoo?

[4]
Yatupwe yalipo na takataka,
Na uoshwe kwa damu ya kondoo
Huoni kijito cha tiririka
Na uoshwe kwa damu ya kondoo?

[chorus]
Kuoshwa, kwa damu
Itutakasayo ya kondoo;
Ziwe safi nguo nyeupe mno;
Umeoshwa kwa damu ya kondoo?