Baba Yetu Aliye Mbinguni

[1]
Baba yetu aliye mbinguni
Amenifurahisha yakini
Kuniambia mwake chuoni
Ya kuwa nami Yesu pendoni

[chorus]
Anipenda Mwokozi Yesu
Anipenda, anipenda
Anipenda Mwokozi Yesu
Anipenda mimi

[2]
Nimwachapo kutanga mbali
Yeye yu vivyo hupenda kweli
Hunirejeza kwake moyoni
Kweli yu nami Yesu pendoni

[chorus]
Anipenda Mwokozi Yesu
Anipenda, anipenda
Anipenda Mwokozi Yesu
Anipenda mimi

[3]
Anipenda! nami nampenda
Kwa wokovu alionitenda
Akanifia msalabani
Kwa kua nami Yesu pendoni

[chorus]
Anipenda Mwokozi Yesu
Anipenda, anipenda
Anipenda Mwokozi Yesu
Anipenda mimi

[4]
Haya kujua yanipa raha
Kumwamini kuna furaha
Humfukuza mara shetani
Kwona yu nami Yesu pendoni

[chorus]
Anipenda Mwokozi Yesu
Anipenda, anipenda
Anipenda Mwokozi Yesu
Anipenda mimi

[5]
Sifa ni nyingi asifiwazo
Moja ni sana katika hizo
Wala siachi hata mbinguni
Kwimba " Yu nami Yesu pendoni "

[chorus]
Anipenda Mwokozi Yesu
Anipenda, anipenda
Anipenda Mwokozi Yesu
Anipenda mimi