Njooni Na Furaha

Language: Swahili
Nyimbo Za Umoja

Njooni Na Furaha

[1]
Njoni na furaha, enyi wa imani,
Njoni Bethlehemu upesi!
Amezaliwa jumbe la Mbinguni
Njoni tumuabudu, Njoni tumabudu,
Njoni tumuabudu Mwokozi.

[2]
Mungu wa waungu, Mwanga wa mianga,
Amekuwa radhi kuzaliwa:
Mungu wa kweli, wala si kiumbe
Njoni tumuabudu, Njoni tumuabudu,
Njoni tumuabudu Mwokozi.

[3]
Jeshi la mbinguni, Imbeni kwa nguvu!
Mbingu zote na zijae sifa!
Sifuni Mungu aliye mbinguni;
Njoni tumuabudu, Njoni tumuabudu,
Njoni tumuabudu Mwokozi.