Naendea Msalaba

Language: Swahili
Nyimbo Za Umoja

Naendea Msalaba

[1]
Naendea msalaba
Ni mnyonge na mpofu
Yapitayo naacha
Nipone msalabani

[chorus]
Nakutumaini tu,
Ewe Mwana wa Mungu
Nainamia kwako
Niponye, mponya wangu

[2]
Nakulilia sana
Nalemewa na dhambi
Pole Yesu asema
Nitazifuta zote

[chorus]
Nakutumaini tu,
Ewe Mwana wa Mungu
Nainamia kwako
Niponye, mponya wangu

[3]
Natoa vyote kwako
Nafasi nazo nguvu
Roho yangu na mwili
Viwe vyako milele

[chorus]
Nakutumaini tu,
Ewe Mwana wa Mungu
Nainamia kwako
Niponye, mponya wangu

[4]
Kwa damu yake sasa
Nimegeuka roho
Nikaziacha tamaa
Nimfuate Yesu

[chorus]
Nakutumaini tu,
Ewe Mwana wa Mungu
Nainamia kwako
Niponye, mponya wangu