Mwamba Wenye Imara

[1]
Mwamba wenye imara, kwako nitajificha!
Maji hayo na damu, yaliyotoka humu,
Hunisafisha dhambi, hunifanya mshindi.

[2]
Kwa kazi zote pia, sitimizi sheria
Nijapofanya bidii, nikilia na kudhii,
Hayaishi makosa, ndiwe wa kuokoa.

[3]
Sina cha mkononi, naja msalabani
Nili tupu nivike, ni mnyonge nishike,
Nili mchafu naja, nioshe nisijafa.

[4]
Nikungojapo chini, nakwenda kaburini
Nipaapo mbinguni, na kukwona enzini,
Roho yangu na iwe, rahani mwako wewe.