ZILETENI ZAKA KWA HAZINA

[1]
Sikieni neno la Mungu wetu, zileteni zaka kwa hazina
Leteni na mioyo yenu yote; mibaraka itakuja.

Chorus
Zileteni zaka kwa hazina, kanijaribu sasa nazo;
Nitakupeni mibaraka, zaidi ya nafasi ya kupewa.

[2]
Wakati Roho Mtakatifu kwako? Uzilete zaka kwa hazina
Ukae karibu na Bwana wako, ndipo utabarikiwa.

[3]
Je,una kasoro na Bwana wako? Uzilete zaka kwa hazina,
Uzilete kama alivyo sema, Ndipo utabarikiwa.

[4]
Ushukuru Bwana na moyo wote, unapo leta zaka ghalani;
Usadiki ahadi zake zote, ndipo utabarikiwa.

[5]
Tuimbe sote nyimbo za furaha, tunapoleta zaka ghalani
Twimbe kabisa na furaha kubwa, kwani tutabarikiwa.

09[5]