MIGUUNI PAKE YESU

[1]
Miguuni pake Yesu, Maneno yake tamu;
Pahali palipo heri, Niwepo kila siku.
Miguuni pake Yesu, Nakumbuka upendo
Nahisani vyake kwangu, Vimenivuta moyo.

[2]
Miguuni pake Yesu, Hapa pahali bora
Pakuweka dhambi zangu, Pahali pa pumziko.
Miguuni pake Yesu, Hapa nafanya sala,
Kwake napewa uwezo, Faraja na nehema.

[3]
Unibariki Mwokozi, Ni miguuni pako,
Unitazame kwa pendo, Nione uso wako.
Nipe Bwana nia yake, Ili ionekane
Nimekaa na Mwokozi, Aliye haki yangu.

04[6]