ANAKUJA UPESI

Language: Swahili
Nyimbo Za Kikristo

ANAKUJA UPESI

[1]
Anakuja upesi, Yesu Bwana wetu,
Msafiri mbali na kwao;
Alisema dhahiri, ‘Nitakuja tena‘;
Amina; na uje, E Bwana.

Chorus
Yuaja, Yesu atarudi sasa;
Anakuja duniani.
Wasafiri wote watapumzika,
Yesu anaporudi tena.

[2]
Makaburi yote wafu wanapolala,
Yatafunguliwa tena;
Na mamilioni pale wataondoka tena,
Wasione machozi kamwe.

[3]
Hatutatengana na hao tena huko;
Nyimbo nzuri tutaimba.
Watakusanyika `toka kila kabila,
Miguuni pa Mwana-Kondoo.

[4]
Aleluya Amin! Aleluya tena!
Upendo wake unashinda!
Tutamsifu milele, hata tutashangaa,
Jinsi alivyotukomboa.

15[9]