KAZI YANGU IKIISHA

Song Lyrics

KAZI YANGU IKIISHA

Nyimbo Za Kikristo · Swahili
Present

Lyrics

Font size:
[1]
Kazi yangu ikisha,nami nikiokoka;
Na kuvaa kutokuharibika,
Nitamjua mwokozi nifikapo ng`amboni;
Atakuwa wa kwanza kunilaki.

Chorus
Nitamjua,Nitamjua,nikimwona uso kwa uso;
Nitamjua,Nitamjua,kwa alama za misumari.

[2]
Furaha nitapata nikiona makao`
Bwana aliyotuandalia;
Nitamsifu Mwokozi kwa rehama na pendo;
Vilivyonipa pahali mbinguni.

[3]
Nao waliokufa katika Bwana Yesu,
Nitawaona tena huko juu;
Lakini nifikapo kwake huko mbinguni,
Nataka kumwona Mwokozi kwanza.

[4]
Milangoni mwa mji Bwana atanipisha,
Pasipo machozi wala huzuni.
Nitauimba wimbo wa milele;lakini
Nataka kumwona mwokozi kwanza.

17[7]

Support My Songbooks

Help us expand our library and keep the music alive for everyone. Even a small donation goes a long way.

Buy me a coffeeBuy us a coffee