U MWENDO GANI NYUMBANI

[1]
U mwendo gain nyumbani? Mlinzi akanijibu,
‘Usiku sasa waisha, macheo karibu.‘
Usihuzunike tena, bali ulemee mwendo
Hata ushike ufalme kule mwangani juu.

[2]
Na tena niliuliza, nchi yote ikajibu;
‘Sasa mwendo watimika, milele karibu.‘
Usihuzunike tena, ishara kuu zasonga
Na viumbe vyangojea sauti ya Bwana.

[3]
Nikamwuliza shujaa, ndivyo kanitia moyo:
‘Shikilia mapigano, kitambo yaisha.‘
Usihuzunike tena, kazi ifanywe kwa moyo;
Tumeahidiwa tunu tuishapo shinda.

[4]
Siyo mbali na nyumbani! Fikira tamu njiani,
Latupoza roho, nalo lafuta machozi.
Usihuzunike tena, kitambo tutakutana
Wenye furaha kamili nyumbani mwa Baba

15[8]