YANIPASA KUWA NAYE

[1]
Yanipasa kuwa naye, Mwokozi Bwana wangu.
Akiwa karibu nami, napata nguvu kweli.

Chorus
Moyo hauogopi, wala kutikisika.
Nitakwenda apendapo, kwa kuwa anilinda.

[2]
Yanipasa kuwa naye, kwani nategemea;
Anaweza kufariji na maneno matamu.

[3]
Yanipasa kuwa naye maisha yangu yote;
Yakiwapo majaribu na mashaka yo yote.

[4]
Yanipasa kuwa naye katika njia zangu;
Macho yake yaongoza hatua zangu zote.

15[4]