WAMWENDEA YESU

[1]
Wamwendea Yesu kwa kusafiwa. Kuoshwa kwa damu ya Kondoo?
Je, neema yake yatumwagiwa? Waoshwa kwa damu ya Kondoo?

Chorus
Kuoshwa kwa damu Itutakasayo ya Kondoo?
Ziwe safi nguo nyeupe sana; Waoshwa kwa damu ya Kondoo?

[2]
Wamwandama daima Mkombozi. Waoshwa kwa damu ya Kondoo?
Yako kwa Msulubiwa mavazi? Waoshwa kwa damu ya Kondoo?

[3]
Atakapokuja Bwana-arusi Uwe safi katika damu!
Yafae kwenda mbinguni mavazi: Yaoshwa kwa damu ya Kondoo?

[4]
Yatupwe yalipo na takataka; Uoshwe kwa damu ya Kondoo:
Huoni kijito chatiririka Uoshwe kwa damu ya Kondoo?

11[7]