UNIVUTE KARIBU

[1]
Univute karibu, Baba, Unikumbatie;
Unisongeze kifuani, Nataka pumziko.

Chorus
Univute karibu (Vuta, univute karibu)
Kwa kamba za upendo, (Kwa kamba, kamba za upendo)
Univute (Kwa kamba za upendo, Univute karibu)
Karibu nawe. (Univute karibu)

[2]
Univute Mwokozi wangu, Na tusiachane;
Mikono yako juu yangu Leo niione.

[3]
Univute kwa Roho yako, Nifanane nawe;
Unioshe, unihuishe, Niwe safi, huru.

14[8]