UKINGONI MWA TORDANI

[1]
Ukingoni mwa Yordani ninaangalia
Bara nzuri ya Kanaani, ninayotamani.

Chorus
Tutakaa pamoja na Yesu, Katika pwani yenye raha;
Tutaimba wimbo wa Musa na Kondoo, Milele hata milele.

[2]
Bara ile ina nuru, nuru ya milele;
Kristo, Jua, hutawala, hufukuza giza.

[3]
Nitapafikia lini na kubarikiwa,
Penye ufalme wa Baba, na kumwona uso?

[4]
Furaha yangu rohoni ni kuchukuliwa;
Siyaogopi mawimbi katika Yordani.

17[8]