UISHI NDANI YANGU

[1]
Tawala ndani yangu, Ee Yesu, Mfalme.
Uwe kwangu majibu Kwa maswala yangu;
Uishi ndani yangu, Wewe, mwongozi
Utumishi ni wangu, Wako utukufu.

[2]
Hekalu nimetoa, Umelisafisha;
Sasa fahari yako Imulike ndani;
Dunia iwe kimya, Mwili sasa uwe
Mtumwa mtulivu Wa kukutii tu.

[3]
Viungo vyake mwili, Vyote vikungoja
Tayari vikiitwa Kwenda, kusimama;
Bila manung`uniko Au malaumu,
Au kusumbuliwa, Pasipo majuto.

[4]
Niwe na utulivu Pasipo haraka;
Tayari kungojea Maagizo yake.
Tawala ndani yangu. Ee Yesu, Mfalme,
Uwe kwangu majibu Kwa maswali yote.

14[7]