ATI TUONANE MTONI

[1]
Ati tuonane mtoni? Maji mazuri ya mbingu;
Yanatokea mwangani, penye kiti cha Mungu.

Chorus
Naam, tuonane mtoni! Watakatifu, kwenu ni mtoni!
Tutakutanika kule mtoni penye kiti cha Mungu.

[2]
Tukitembea mtoni na Yesu Mchunga wetu,
Daima tu ibadani usoni pake kwetu.

[3]
Tukisafiri mtoni tutue ulemeao
Wema wa Mungu yakini; una taji na yao!

[4]
Kwang`ara sana mtoni cha Mwokozi ni kioo,
Milele hatuachani tumsifu kwa nyimbo.

[5]
Karibu sana mtoni, karibu tutawasili,
Mara huwa furahani na amani ya kweli.

17[6]