TWENDENI ASKARI

[1]
Twendeni askari, Watu wa Mungu;
Yesu yuko mbele, Tumwandame juu;
Ametangulia Bwana vitani,
Twende mbele kwani ndiye amini.

Chorus
Twendeni Askari, Watu wa Mungu;
Yesu yuko mbele, Tumwandame juu;

[2]
Jeshi la shetani, likisikia
Jina la Mwokozi, litakimbia;
Kelele za shangwe zivume pote;
Ndugu, inueni zenu sauti.

[3]
Kweli kundi dogo, watu wa Mungu,
La mababa yetu ni letu fungu;
Hatutengwi nao, moja imani;
Tumaini moja, na moja dini.

[4]
Haya mbele watu nasi njiani,
Inueni myoyo, nanyi sifuni;
Heshima na sifa yake Mfalme;
Juu hata chini sana zivume.

06[5]