TUSIMAME IMARA MWAMBANI

[1]
Umtetee Mungu duniani ijapo pepo kali za vuma;
Mwambani pekee pana nguvu Dhambi ikimea.

Chorus
Tusimame imara katika mwamba,
Mwamba wa Kristo pekee;
Ndipo salamini tutasimama
Kule kitini pa enzi.

[2]
Itetee haki kwa bidii, kwa moyo mnyofu wa imani;
Mwambani pekee utashinda wingi wa upotovu.

[3]
Itetee kweli, itadumu, ijapo kawia itashinda;
Mwambani pekee pana raha yaishapo tufani.

06[8]