TUMESIKIA MBIU

[1]
Tumesikia mbiu: Yesu huokoa; Utangazeni kote, Yesu huokoa.
Tiini amri hiyo: nchini baharini. Enezeni mbiu hii: Yesu huokoa.

[2]
Imba nawe askari: Yesu huokoa Kwa nguvu ya kombozi, Yesu huokoa.
Imbeni wenye shida, unapoumwa moyo, Na kaburini imba: Yesu huokoa.

[3]
Mawimbini uenee. Yesu huokoa; Wenye dhambi jueni: Yesu huokoa;
Visiwa na viimbie, vilindi itikeni, Na nchi shangilie: Yesu huokoa.

[4]
Upepo utangaze: Yesu huokoa; Mataifa yashangaa: Yesu huokoa.
Milimani, bondeni, sauti isikike Ya wimbo wa washindi: Yesu huokoa.

10[8]