TAFUTA DAIMA UTAKATIFU

[1]
Tafuta daima utakatifu;
Fanya urafiki na Wakristo tu;
Nena siku zote, na Bwana wako,
Baraka uombe kwa kila jambo.

[2]
Tafuta daima utakatifu;
Uwe peke yako ukimwabudu;
Ukimwangalia Mwokozi wako,
Utabadilishwa kama alivyo.

[3]
Tafuta daima utakatifu;
Kiongozi wako awe Yesu tu;
Katika furaha au huzuni,
Dumu kumfuata Yesu Mwokozi.

[4]
Tafuta daima utakatifu;
Umtawaze Roho moyoni mwako,
Akikuongoza katika haki,
Hufanywa tayari kwa kazi yake.

13[4]