TABIBU MKUU

Language: Swahili
Nyimbo Za Kikristo

TABIBU MKUU

[1]
Tabibu mkuu huyu, Yesu mwenye huruma
Atuletaye faraja: Yesu, Mwokozi wetu.

Chorus
Imbeni, Malaika, SIfa za Bwana wetu:
Jina la pekee kwetu, ni la Yesu Bwana.

[2]
Mwana Kondo-o msifuni Mwokozi;
Hatia zote na dhambi, Huziondoa Yesu.

[3]
Hakuna jina jingine, Linalofa-a sifa;
A-u kutufurahisha, Isipokuwa lake.

[4]
Naye atakapokuja, Na utukufu wake;
Tutafurahi milele, Kuka-a kwake Bwana.

11[1]