ROHO YANGU AMKA SASA

[1]
Roho yangu amka sasa, mara jitahidi;
Shindano ni lake Bwana, zawadi ni taji.

[2]
Sauti ni yake Mungu inayokuita;
Ndiyo aliyekirimu taji ya uzima.

[3]
Mashaidi ndio wengi wanao kuona;
Ya nyuma usifikiri bali mwendo kaza.

[4]
Bwana umetuanzisha katika shindano;
Kwa vile tunaposhinda ushindi ni wako.

06[6]