RAHA YANGU YOTE, BWANA

[1]
Raha yangu yote, Bwana, I mbavuni pako;
Mimi sina haja tena ila kifo chako.

[2]
Mwokozi uliyekufa, nawe ndiwe Mungu,
Kifo chako ni kwa dhambi, ziondoe zangu.

[3]
Nioshe na niwe wako, nawe uwe wangu;
Nioshe damuni mwako liwe fungu langu.

[4]
Nioshe si miguu tu, osha tangu nyayo,
Hata kichwa changu juu, na ndani ya moyo,

[5]
Na iwe kafara damu nifanyapo kazi,
Hata imani itimu, nikwone,Mwokozi.

190