PENDO LAKO, EE MWOKOZI

[1]
Pendo lako , Ee Mwokozi, Hushinda pendo zote!
Kaa nasi, ndani yetu, Furaha ya mbinguni.
Yesu, u rehema tupu, Safi, na kusamehe,
Mfariji mwenye huzuni Ziondoe machozi.

[2]
Roho yako ya upendo Tuma kwa kundi lako;
Hebu tuirithi raha, Iliyoahidiwa.
Uondoe moyo mbaya, U Mwanzo, tena Mwisho;
Timiza imani yetu, Ilituwekwe `huru.

[3]
Yesu, uje kwetu sasa, Tupokee huruma;
Rudi kwetu, tena kamwe Usituache pekee.
Tungekutukuza leo, pamoja na malaika,
Imba na kutoa sifa, Ingia kwa ibada.

[4]
Sasa, Bwana, kazi yako, Imalize moyoni;
Takasa hekalu lako, Wokovu kamilisha!
Safisha viumbe vyako Katika wakati huu;
Tupumzike `toka dhambi, Tuingie mbinguni.

03[7]