NIUONAPO MSALABA

[1]
Niuonapo msalaba, Kristo aliponifilia;
Kwangu pato ni hasara. Kiburi nakichukia.

[2]
Na nisijivune, Bwana, Ila kwa sadaka yako;
Upuzi sitaki tena, Zi chini ya damu yako.

[3]
Tangu kichwa hata nyayo, Zamwagwa pendo na hamu,
Ndako pweke hamu hiyo. Pendo zako zimetimu.

[4]
Vitu vyote vya dunia, Si sadaka ya kutosha;
Pendo zako zaniwia, Nafsi, mali, na maisha.

06[3]