NIMEKOMBOLEWA NA YESU

[1]
Nimekombolewa na Yesu na sasa nimefurahi;
Kwa bei ya mauti yake mimi ni mtoto wake.

Chorus
Kombolewa! Nakombolewa na damu;
Kombolewa! mimi mwana wake kweli.

[2]
Kukombolewa nafurahi, kupita lugha kutamka;
Kulionyesha pendo lake, mimi ni mtoto wake.

[3]
Nitamwona Mfalme wangu, katika uzuri wake;
Ambaye najifurahisha katika torati yake.

[4]
Najua taji imewekwa mbinguni tayari kwangu;
Muda kitambo atakuja, ili alipo, niwepo.

03[5]