NILIPOTOKA KABISA

[1]
Nilipotoka kabisa, sasa narudi;
Nikakawia dhambini, Bwana narudi.

Chorus
Narudi nyumbani: daima kwako.
Kwa upendo nipokee: Naja nyumbani.

[2]
Nikasusurika sana, sasa narudi;
Mwenye uchungu natubu, Bwana narudi.

[3]
Nimechoka maovuni, sasa narudi;
Pendo lako lanivuta, Bwana narudi.

[4]
Ndilo tumaini langu, sasa narudi;
Yesu alinifilia, Bwana narudi.

[5]
Damu yake yanitosha, sasa narudi;
Unioshe kenyekenye, Bwana narudi.

11[8]