NIAMBIE, EE MLINZI

[1]
Niambie, Ee mlinzi, Umepambazuka je!
Utukufu wa Zayini, Pana dalili zake?
Msafiri uondoke, Utazame mbinguni,
Kiunoni ujifunge, Ni kucha alfajiri.

[2]
Mlinzi inamulika Nuru njiani mwako,
Dalili za kuja kwake, Kwamba siku karibu;
Panda itakapolia Itawaamsha wafu,
Watakatifu wa Mungu, Kuwapa kutokufa.

[3]
Mlinzi, ione nuru Ya mwaka wa Sabato;
Sauti zinatangaza Ufalme ni karibu;
Msafiri ninaona Mlima wa Zayuni,
Mji wa Yerusalemi Nayo fahari yake.

[4]
Kwenye mji wa dhahabu Anaketi mfalme
Katika kiti kizuri: huku anatawala.
Pana amani po pote, Mashamba husitawi;
Na ardhi ina rutuba; Mito ni mitulivu.

[5]
Mlinzi, twaribia Nchi iliyo nzuri;
Twende mbele, tufurahi, Nchi inachangamka,
Sikieni kuna wimbo Wa waliookoka;
Kaza mwendo, Ujiunge Na kundi Kubwa hili.

07[4]