NI SALAMA ROHONI MWANGU

[1]
Nionapo amani kama shwari, au nionapo shida;
Kwa hali zote umenijulisha ni salama rohoni mwangu.

Chorus
Salama rohoni, Ni salama rohoni mwangu.

[2]
Ingawa shetani atanitesa, nitajipa moyo kwani,
Kristo ameona unyonge mwangu; amekufa kwa roho yangu.

[3]
Dhambi zangu zote, wala si nusu, huwekwa msalabani;
Wala sichukui laana yake, ni salama rohoni mwangu.

[4]
Ee Bwana himiza siku ya kuja, panda itakapolia:
Utakaposhuka sitaogopa ni salama rohoni mwangu.

12[7]