NATAKA IMANI HII

[1]
Nataka Imani hii: Imani imara,
Ambayo haitetemi Kitu chote
Wakati wa shida,
Wakati wa shida.

[2]
Isiyonung`unika Huzuni, taabu;
Lakini katika saa ya matata
Humwamini Mungu,
Humwamini Mungu.

[3]
Imani inayo ng`aa katika tufani;
Isiyoogopa giza, wala shida,
Njaa na Hatari,
Njaa na hatari.

[4]
Haiogopi dunia, Kudharau kwake;
Haiangushwi na hila, na uwongo
Dhambi na ogofyo,
Dhambi na ogofyo.

[5]
Bwana, nipe imani hii, Hivi nitaweza
Kuonja hapa chini ulimwenguni,
Kurithi furaha,
Kurithi furaha.

07[9]