NASIFU SHANI YA MUNGU

[1]
Nasifu shani ya Mungu, mweneza bahari,
Muumba pia wa mbingu, jua, nyota, mwezi,
Ni tukufu yako shani, mtengeza mambo
Ya nyakati na zamani, yasiyo na mwisho.

[2]
Kadri ya nionayo, ya kusifu Mungu;
Nchi niikanyagayo, na hayo mawingu;
Hakuna hata unyasi, usiokuza;
Na upepo wavumisha, au kutuliza.

[3]
Nami kwa mkono wako, naongozwa sawa,
Ni pato nikusifupokukwomba ni dawa;
Umenizingira nyuma, na mbele baraka;
Maarifa ya ajabu! Yanishinda mimi!

03[8]