NAPENDA KITABU CHAKE

[1]
Napenda kitabu chake, kilichotoka mbinguni,
Barua kwangu ya Bwana Ujumbe wake wa`pendo.

[2]
Humo ndani ya kitabu Sura ya Yesu naona;
Karatasi zimekuwa, Wayo zake za Mwongozi.

[3]
Mapenzi yake Mwumbaji, Kubwe la asali tamu;
Natamani kuuonja, Ule mkate wa uzima.

[4]
Mapenzi Yake Mwumbaji, Yanafunuliwa humo;
Hazina kuu ya hekima, Utajiri wa ajabu.

[5]
Mwangaza wa ulimwengu Angaza humo moyoni!
Uwe mwandamizi pote, Taa ya hatua zangu.

06[2]