NAMTAKA BWANA YESU

[1]
Ulimwengu siutaki, Namtaka Bwana Yesu;
Dunia hunidanganya; Yesu yu mwaminifu.

Chorus
Rehema ni ya ajabu! Pendo bila kipimo!
Wokovu mkamilifu, Amana ya uzima!

[2]
Ulimwengu siutaki, Namtaka Bwana Yesu;
Kati ya dhoruba kali Yenye wimbo mtamu.

[3]
Ulimwengu siutaki, Namtaka Bwana Yesu;
Safarini duniani Yeye furaha yangu.

[4]
Ulimwengu siutaki, Namtaka Bwana Yesu;
Msalaba naamini, Hata namwona Yesu.

14[5]