NAENDEA MSALABA

[1]
Naendea msalaba, Ni mnyonge, mpofu,
Yapitayo naacha nipe msalaba tu.

Chorus
Nakutumaini tu, ewe Mwana wa Mungu;
Nainamia kwako; niponye sasa, Bwana.

[2]
Nakulilia sana: nalemewa na dhambi;
Pole Yesu asema: ‘Nitazifuta zote.‘

[3]
Natoa vyote kwako, nafasi nazo nguvu,
Roho yangu na mwili viwe vyako milele.

[4]
Kwa damu yake sasa amenivuta sana,
Upendo hubidisha, nimtafute Mwokozi.

11[5]