MWAMBA WENYE IMARA

[1]
Mwamba wenye imara,kwako nitajificha!
Maji hayo na damu yaliyotoka humu,
Hunisafi na dhambi,Hunifanya m-shindi.

[2]
Kwa kazi zote pia sitimizi sheria,
Nijapofanya bidii,nikilia na kudhii,
Hayaishi makosa;ndiwe wa kuokoa.

[3]
Sina cha mkononi,naja msalambani,
Nili tupu,nivike;ni mnyonge,nishike;
Nili mchafu,naja,nioshe nisijafa.

[4]
Nikungojapo chini,na kwenda kaburini,
Nipaapo mbinguni na kukwona enzini,
Roho yangu na iwe rahani mwako wewe

19[2]