MSALABANI PA MWOKOZI

[1]
Msalabani pa Mwokozi Hapo niliomba upozi,
Moyo wangu ulitakaswa, Na asifiwe.

Chorus
Na asifiwe, Na asifiwe,
Alinikomboa kwa damu, Na asifiwe.

[2]
Chini ya mti msumbufu Niliomba utakatifu,
Alinikomboa kwa damu, Na asifiwe.

[3]
Kwa ajabu nina okoka, Yesu anakaa moyoni;
Mtini alinifia, Na asifiwe.

[4]
Damu ya Yesu ya dhamani Huniokoa makosani;
Huniendesha wokovuni, Na asifiwe.

01[9]