MPAKA LINI BWANA

[1]
Mpaka lini Bwana, Utakaa mbali?
Kumetuchosha moyo kukawia hivi.
Utatujia lini, Ili tufurahi
Katika ile nuru, kuja kutukufu?

[2]
Mpaka lini Yesu, Utaacha watu
Uliowakomboa, Wawe na mashaka?
Wachache waamini, Kwamba utarudi;
Wachache wa tayari, Bwana kukulaki.

[3]
Waamshe watu wako, Tangaza kilio:
‘Mwe watakatifu, Bwanayu karibu!‘
Utatujia lini, Ili tufurahi
Katika ile nuru, Kutukufu?

07[8]