MFALME YU MLANGONI

[1]
Mfalme yu mlangoni, Ndiye aliyetufia;
Mara wote wampendao atawakusanya.

Chorus
Yuaja, yuaja, mlangoni anasimama;
Anakuja, anakuja, Kuja kwake karibu.

[2]
Dalili za kuja kwake Zinazidi kutimizwa;
Karibu wateule watamlaki Bwana.

[3]
`Sitafute duniani amani wala furaha,
Mpaka Bwana arudi dhambi kuondoa.

[4]
Tutakaa na Mwokozi Makaoni ya milele;
Daima tutafurahi kuwa watu wake.

15[7]