MAPYA NI MAPENZI

[1]
Mapya ni mapenzi hayo,
Asubuhi tuonayo;
Saa za giza hulindwa,
Kwa uzima kuamka.

[2]
Kila saku, mapya pia,
Rehema, wema na afya,
Wokovu na msamaha,
Mawazo mema, furaha.

[3]
Tukijitahidi leo
Na mwendo utupasao,
Mungu atatueleza
Yatakayompendeza.

[4]
Mamboyetu ya dunia
Bwana atayang‘aria,
Matata atageuza
Yawe kwetu ya baraka.

[5]
Yaliyo madogo, haya
Bwana tukimfanyia,
Yatosha: tutafaidi
Huvuta kwake zaidi.

[6]
Ewe Bwana, siku zote,
Tusaidie kwa yote:
Mwendo wetu wote vivyo,
Uwe kama tuombavyo.

090