KATIKA WENYE DHAMBI

[1]
Katika wenye dhambi,
Ndimi mkuu wao-
Ila Yesu ukaja,
Kwa dhambi alikufa,
Akamimina damu,
Niupate uzima.

[2]
Ajabu! Pendo lake!
Pendo lililo kuu,
Pendo lisilo mwisho,
Lidumulo milele-
Lililonitafuta
Ingawa sikumpenda

[3]
Ingawa ni mbaya
Kristo ni vyote kwangu;
Ajua haja zangu;
Huzuni zangu, zake;
Hata katika vita,
Akiwapo Salama.

12[1]