JUA LA ROHONI MWANGU

[1]
Jua la rohoni mwangu, mpendwa Mwokozi wangu;
Usiku giza hapana, ukiwa karibu Bwana

[2]
Nikipata usingizi, nijaze fikira hizi,
Nitamu sana, nilale pendoni mwako milele.

[3]
Kaa nami, ewe Bwana, usiku kama mchana,
Nisiishi mbali nawe; ni uhai kuwa nawe.

[4]
Kama mtotomnyonge ameshawishwa atange,
Mtafute Ewe Bwana, ujirudishie tena.

[5]
Wagonjwa wape amani, waneemeshe maskini,
Waliao, Mtulizi, wape wote usingizi.

[6]
Asubuhi tutokapo, tukaribie tulipo;
Twingiapo duniani tuwe mwako mkononi.

09[3]