HUNA KITU KWA YESU

[1]
Ukitafuta mali, Huna wasaa kwa Yesu?
Kwa matendo ya haki Huna wasaa kwa Yesu?
Anasa za dunia, Mambo yako ya raha
Haya unatafuta; Huna wasaa kwa Yesu?

[2]
Mambo yanakusonga: Kwakehuna nafasi?
Watekwa na dunia, Kwake huna nafasi?
Humwona m-langoni, Anapopiga hodi?
Daima hukusihi: Kwake huna nafasi?

[3]
Sa-a ni za thamani, Kwake hamnayo kazi
Wala hamfanyi bidii, Kwake hamnayo kazi?
Hamkufikia kwao Waliomo shimoni
Na waliopotea? Kwake hamnayo kazi?

[4]
Na wazaa majani tu? Huna tunda kwa Yesu?
Mikono I mitupu, Huna tunda kwa Yesu?
Huna chembe kwa ghala Kazi yako kulipa;
Wala huna furaha Unapomwona Yesu?

10[6]