HATUTAAGANA TENA

[1]
Tuonanapo na rafiki sote twafurahi,
Ila tumepaswa mwishowe kuagana tena.

Chorus
Hatutaagana tena nyumbani mbinguni,
Kwenye nchi tamu juu, Hatutaagana.

[2]
Twatumaini kwa furaha tutaonana juu
Na rafiki tulioaga tuishapo shinda.

[3]
Kule hatutatamka kamwe neno la kuaga,
Tutaimba daima tena nyimbo za furaha.

18[6]